Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Beyyine 1 / 8
1
Hawakuwa walio kufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina waache walio nayo mpaka iwajie bayana,
Barwani 98:1
2
Yaani Mtume aliye toka kwa Mwenyezi Mungu anaye wasomea kurasa zilizo takasika,
Barwani 98:2
3
Ndani yake mna maandiko yaliyo nyooka.
Barwani 98:3
4
Wala hawakufarikiana walio pewa Kitabu ila baada ya kuwajia hiyo bayana.
Barwani 98:4
5
Nao hawakuamrishwa kitu ila wamuabudu Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia Dini, wawe waongofu, na washike Sala, na watoe Zaka. Na hiyo ndiyo Dini madhubuti.
Barwani 98:5
6
Hakika walio kufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina wataingia katika Moto wa Jahannamu wadumu milele humo. Hao ndio viumbe waovu kabisa.
Barwani 98:6
7
Hakika walio amini na wakatenda mema, hao ndio bora wa viumbe.
Barwani 98:7
8
Malipo yao kwa Mola wao Mlezi ni Bustani za daima, zipitazo mito kati yake. Wakae humo milele. Mwenyezi Mungu yu radhi nao, na wao waradhi naye. Hayo ni kwa anaye mwogopa Mola wake Mlezi.
Barwani 98:8
Beyyine suresi tamamlandı