Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Alak 1 / 19
1
Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,
Barwani 96:1
2
Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,
Barwani 96:2
3
Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!
Barwani 96:3
4
Ambaye amefundisha kwa kalamu.
Barwani 96:4
5
Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.
Barwani 96:5
6
Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri
Barwani 96:6
7
Akijiona katajirika.
Barwani 96:7
8
Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.
Barwani 96:8
9
Umemwona yule anaye mkataza
Barwani 96:9
10
Mja anapo sali?
Barwani 96:10
11
Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?
Barwani 96:11
12
Au anaamrisha uchamngu?
Barwani 96:12
13
Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?
Barwani 96:13
14
Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?
Barwani 96:14
15
Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!
Barwani 96:15
16
Shungi la uwongo, lenye makosa!
Barwani 96:16
17
Basi na awaite wenzake!
Barwani 96:17
18
Nasi tutawaita Mazabania!
Barwani 96:18
19
Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!
Barwani 96:19
Alak suresi tamamlandı