1
Hatukukunjulia kifua chako?
2
Na tukakuondolea mzigo wako,
3
Ulio vunja mgongo wako?
4
Na tukakunyanyulia utajo wako?
5
Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi,
6
Hakika pamoja na uzito upo wepesi.
7
Na ukipata faragha, fanya juhudi.
8
Na Mola wako Mlezi ndio mshughulikie.