Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Şems 1 / 15
1
Naapa kwa jua na mwangaza wake!
Barwani 91:1
2
Na kwa mwezi unapo lifuatia!
Barwani 91:2
3
Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
Barwani 91:3
4
Na kwa usiku unapo lifunika!
Barwani 91:4
5
Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
Barwani 91:5
6
Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
Barwani 91:6
7
Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
Barwani 91:7
8
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,
Barwani 91:8
9
Hakika amefanikiwa aliye itakasa,
Barwani 91:9
10
Na hakika amekhasiri aliye iviza.
Barwani 91:10
11
Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,
Barwani 91:11
12
Alipo simama mwovu wao mkubwa,
Barwani 91:12
13
Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.
Barwani 91:13
14
Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.
Barwani 91:14
15
Wala Yeye haogopi matokeo yake.
Barwani 91:15
Şems suresi tamamlandı