Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Beled 1 / 20
1
Naapa kwa Mji huu!
Barwani 90:1
2
Nawe unaukaa Mji huu.
Barwani 90:2
3
Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.
Barwani 90:3
4
Hakika tumemuumba mtu katika taabu.
Barwani 90:4
5
Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?
Barwani 90:5
6
Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.
Barwani 90:6
7
Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?
Barwani 90:7
8
Kwani hatukumpa macho mawili?
Barwani 90:8
9
Na ulimi, na midomo miwili?
Barwani 90:9
10
Na tukambainishia zote njia mbili?
Barwani 90:10
11
Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.
Barwani 90:11
12
Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?
Barwani 90:12
13
Kumkomboa mtumwa;
Barwani 90:13
14
Au kumlisha siku ya njaa
Barwani 90:14
15
Yatima aliye jamaa,
Barwani 90:15
16
Au masikini aliye vumbini.
Barwani 90:16
17
Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.
Barwani 90:17
18
Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.
Barwani 90:18
19
Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.
Barwani 90:19
20
Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.
Barwani 90:20
Beled suresi tamamlandı