Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Fecr 1 / 30
1
Naapa kwa alfajiri,
Barwani 89:1
2
Na kwa masiku kumi,
Barwani 89:2
3
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
Barwani 89:3
4
Na kwa usiku unapo pita,
Barwani 89:4
5
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
Barwani 89:5
6
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?
Barwani 89:6
7
Wa Iram, wenye majumba marefu?
Barwani 89:7
8
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
Barwani 89:8
9
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
Barwani 89:9
10
Na Firauni mwenye vigingi?
Barwani 89:10
11
Ambao walifanya jeuri katika nchi?
Barwani 89:11
12
Wakakithirisha humo ufisadi?
Barwani 89:12
13
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
Barwani 89:13
14
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
Barwani 89:14
15
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
Barwani 89:15
16
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
Barwani 89:16
17
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
Barwani 89:17
18
Wala hamhimizani kulisha masikini;
Barwani 89:18
19
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
Barwani 89:19
20
Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
Barwani 89:20
21
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
Barwani 89:21
22
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
Barwani 89:22
23
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
Barwani 89:23
24
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
Barwani 89:24
25
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
Barwani 89:25
26
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
Barwani 89:26
27
Ewe nafsi iliyo tua!
Barwani 89:27
28
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
Barwani 89:28
29
Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
Barwani 89:29
30
Na ingia katika Pepo yangu.
Barwani 89:30
Fecr suresi tamamlandı