Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Gaşiye 1 / 26
1
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
Barwani 88:1
2
Siku hiyo nyuso zitainama,
Barwani 88:2
3
Zikifanya kazi, nazo taabani.
Barwani 88:3
4
Ziingie katika Moto unao waka -
Barwani 88:4
5
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
Barwani 88:5
6
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
Barwani 88:6
7
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
Barwani 88:7
8
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
Barwani 88:8
9
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
Barwani 88:9
10
Katika Bustani ya juu.
Barwani 88:10
11
Hawatasikia humo upuuzi.
Barwani 88:11
12
Humo imo chemchem inayo miminika.
Barwani 88:12
13
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
Barwani 88:13
14
Na bilauri zilizo pangwa,
Barwani 88:14
15
Na matakia safu safu,
Barwani 88:15
16
Na mazulia yaliyo tandikwa.
Barwani 88:16
17
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
Barwani 88:17
18
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
Barwani 88:18
19
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?
Barwani 88:19
20
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
Barwani 88:20
21
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
Barwani 88:21
22
Wewe si mwenye kuwatawalia.
Barwani 88:22
23
Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,
Barwani 88:23
24
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!
Barwani 88:24
25
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
Barwani 88:25
26
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!
Barwani 88:26
Gaşiye suresi tamamlandı