Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Ala 1 / 19
1
Litakase jina la Mola wako Mlezi aliye juu kabisa,
Barwani 87:1
2
Aliye umba, na akaweka sawa,
Barwani 87:2
3
Na ambaye amekadiria na akaongoa,
Barwani 87:3
4
Na aliye otesha malisho,
Barwani 87:4
5
Kisha akayafanya makavu, meusi.
Barwani 87:5
6
Tutakusomesha wala hutasahau,
Barwani 87:6
7
Ila akipenda Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye anayajua yaliyo dhaahiri na yaliyo fichikana.
Barwani 87:7
8
Na tutakusahilishia yawe mepesi.
Barwani 87:8
9
Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa.
Barwani 87:9
10
Atakumbuka mwenye kuogopa.
Barwani 87:10
11
Na atajitenga mbali nayo mpotovu,
Barwani 87:11
12
Ambaye atauingia Moto mkubwa.
Barwani 87:12
13
Tena humo hatakufa wala hawi hai.
Barwani 87:13
14
Hakika amekwisha fanikiwa aliye jitakasa.
Barwani 87:14
15
Na akakumbuka jina la Mola wake Mlezi, na akasali.
Barwani 87:15
16
Lakini nyinyi mnakhiari maisha ya dunia!
Barwani 87:16
17
Na Akhera ni bora na yenye kudumu zaidi.
Barwani 87:17
18
Hakika haya yamo katika Vitabu vya mwanzo,
Barwani 87:18
19
Vitabu vya Ibrahimu na Musa.
Barwani 87:19
Ala suresi tamamlandı