Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Büruc 1 / 22
1
Naapa kwa mbingu yenye Buruji!
Barwani 85:1
2
Na kwa siku iliyo ahidiwa!
Barwani 85:2
3
Na kwa shahidi na kinacho shuhudiwa!
Barwani 85:3
4
Wameangamizwa watu wa makhandaki
Barwani 85:4
5
Yenye moto wenye kuni nyingi,
Barwani 85:5
6
Walipo kuwa wamekaa hapo,
Barwani 85:6
7
Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini.
Barwani 85:7
8
Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Msifiwa,
Barwani 85:8
9
Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni shaahidi wa kila kitu.
Barwani 85:9
10
Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua.
Barwani 85:10
11
Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
Barwani 85:11
12
Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali.
Barwani 85:12
13
Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejeza tena,
Barwani 85:13
14
Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,
Barwani 85:14
15
Mwenye Kiti cha Enzi, Mtukufu,
Barwani 85:15
16
Atendaye ayatakayo.
Barwani 85:16
17
Je! Zimekuwasilia khabari za majeshi?
Barwani 85:17
18
Ya Firauni na Thamudi?
Barwani 85:18
19
Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha.
Barwani 85:19
20
Na Mwenyezi Mungu nyuma yao amewazunguka.
Barwani 85:20
21
Bali hii ni Qur'ani tukufu
Barwani 85:21
22
Katika Ubao Ulio Hifadhiwa.
Barwani 85:22
Büruc suresi tamamlandı