Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
İnşikak 1 / 25
1
Itapo chanika mbingu,
Barwani 84:1
2
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
Barwani 84:2
3
Na ardhi itakapo tanuliwa,
Barwani 84:3
4
Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,
Barwani 84:4
5
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
Barwani 84:5
6
Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.
Barwani 84:6
7
Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,
Barwani 84:7
8
Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,
Barwani 84:8
9
Na arudi kwa ahali zake na furaha.
Barwani 84:9
10
Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,
Barwani 84:10
11
Basi huyo ataomba kuteketea.
Barwani 84:11
12
Na ataingia Motoni.
Barwani 84:12
13
Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.
Barwani 84:13
14
Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.
Barwani 84:14
15
Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!
Barwani 84:15
16
Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,
Barwani 84:16
17
Na kwa usiku na unavyo vikusanya,
Barwani 84:17
18
Na kwa mwezi unapo pevuka,
Barwani 84:18
19
Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!
Barwani 84:19
20
Basi wana nini hawaamini?
Barwani 84:20
21
Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?
Barwani 84:21
22
Bali walio kufuru wanakanusha tu.
Barwani 84:22
23
Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.
Barwani 84:23
24
Basi wabashirie adhabu chungu!
Barwani 84:24
25
Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.
Barwani 84:25
İnşikak suresi tamamlandı