Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Mutaffifın 1 / 36
1
Ole wao hao wapunjao!
Barwani 83:1
2
Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
Barwani 83:2
3
Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
Barwani 83:3
4
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
Barwani 83:4
5
Katika Siku iliyo kuu,
Barwani 83:5
6
Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?
Barwani 83:6
7
Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.
Barwani 83:7
8
Unajua nini Sijjin?
Barwani 83:8
9
Kitabu kilicho andikwa.
Barwani 83:9
10
Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!
Barwani 83:10
11
Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.
Barwani 83:11
12
Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.
Barwani 83:12
13
Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!
Barwani 83:13
14
Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.
Barwani 83:14
15
Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.
Barwani 83:15
16
Kisha wataingia Motoni!
Barwani 83:16
17
Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.
Barwani 83:17
18
Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.
Barwani 83:18
19
Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?
Barwani 83:19
20
Kitabu kilicho andikwa.
Barwani 83:20
21
Wanakishuhudia walio karibishwa.
Barwani 83:21
22
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.
Barwani 83:22
23
Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.
Barwani 83:23
24
Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,
Barwani 83:24
25
Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,
Barwani 83:25
26
Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.
Barwani 83:26
27
Na mchanganyiko wake ni Tasniim,
Barwani 83:27
28
Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.
Barwani 83:28
29
Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.
Barwani 83:29
30
Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.
Barwani 83:30