Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
İnfitar 1 / 19
1
Mbingu itapo chanika,
Barwani 82:1
2
Na nyota zitapo tawanyika,
Barwani 82:2
3
Na bahari zitakapo pasuliwa,
Barwani 82:3
4
Na makaburi yatapo fukuliwa,
Barwani 82:4
5
Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.
Barwani 82:5
6
Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?
Barwani 82:6
7
Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,
Barwani 82:7
8
Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.
Barwani 82:8
9
Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.
Barwani 82:9
10
Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,
Barwani 82:10
11
Waandishi wenye hishima,
Barwani 82:11
12
Wanayajua mnayo yatenda.
Barwani 82:12
13
Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,
Barwani 82:13
14
Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;
Barwani 82:14
15
Wataingia humo Siku ya Malipo.
Barwani 82:15
16
Na hawatoacha kuwamo humo.
Barwani 82:16
17
Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
Barwani 82:17
18
Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
Barwani 82:18
19
Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.
Barwani 82:19
İnfitar suresi tamamlandı