Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Tekvir 1 / 29
1
Jua litakapo kunjwa,
Barwani 81:1
2
Na nyota zikazimwa,
Barwani 81:2
3
Na milima ikaondolewa,
Barwani 81:3
4
Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,
Barwani 81:4
5
Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,
Barwani 81:5
6
Na bahari zikawaka moto,
Barwani 81:6
7
Na nafsi zikaunganishwa,
Barwani 81:7
8
Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,
Barwani 81:8
9
Kwa kosa gani aliuliwa?
Barwani 81:9
10
Na madaftari yatakapo enezwa,
Barwani 81:10
11
Na mbingu itapo tanduliwa,
Barwani 81:11
12
Na Jahannamu itapo chochewa,
Barwani 81:12
13
Na Pepo ikasogezwa,
Barwani 81:13
14
Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.
Barwani 81:14
15
Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,
Barwani 81:15
16
Zinazo kwenda, kisha zikajificha,
Barwani 81:16
17
Na kwa usiku unapo pungua,
Barwani 81:17
18
Na kwa asubuhi inapo pambazuka,
Barwani 81:18
19
Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,
Barwani 81:19
20
Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,
Barwani 81:20
21
Anaye t'iiwa, tena muaminifu.
Barwani 81:21
22
Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.
Barwani 81:22
23
Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.
Barwani 81:23
24
Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.
Barwani 81:24
25
Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.
Barwani 81:25
26
Basi mnakwenda wapi?
Barwani 81:26
27
Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.
Barwani 81:27
28
Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.
Barwani 81:28
29
Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Barwani 81:29
Tekvir suresi tamamlandı