Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Abese 1 / 42
1
Alikunja kipaji na akageuka,
Barwani 80:1
2
Kwa sababu alimjia kipofu!
Barwani 80:2
3
Na nini kitakujuulisha pengine yeye atatakasika?
Barwani 80:3
4
Au atawaidhika, na mawaidha yamfae?
Barwani 80:4
5
Ama ajionaye hana haja,
Barwani 80:5
6
Wewe ndio unamshughulikia?
Barwani 80:6
7
Na si juu yako kama hakutakasika.
Barwani 80:7
8
Ama anaye kujia kwa juhudi,
Barwani 80:8
9
Naye anaogopa,
Barwani 80:9
10
Ndio wewe unampuuza?
Barwani 80:10
11
Sivyo hivyo! Huku ni kukumbushana.
Barwani 80:11
12
Basi anaye penda akumbuke.
Barwani 80:12
13
Yamo katika kurasa zilizo hishimiwa,
Barwani 80:13
14
Zilizo inuliwa, zilizo takaswa.
Barwani 80:14
15
Zimo mikononi mwa Malaika waandishi,
Barwani 80:15
16
Watukufu, wema.
Barwani 80:16
17
Ameangamia mwanaadamu! Nini kinacho mkufurisha?
Barwani 80:17
18
Kwa kitu gani amemuumba?
Barwani 80:18
19
Kwa tone la manii, akamuumba na akamkadiria.
Barwani 80:19
20
Kisha akamsahilishia njia.
Barwani 80:20
21
Kisha akamfisha, akamtia kaburini.
Barwani 80:21
22
Kisha apendapo atamfufua.
Barwani 80:22
23
La! Hajamaliza aliyo muamuru.
Barwani 80:23
24
Hebu mtu na atazame chakula chake.
Barwani 80:24
25
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu,
Barwani 80:25
26
Tena tukaipasua pasua ardhi kwa nguvu,
Barwani 80:26
27
Kisha tukaotesha humo nafaka,
Barwani 80:27
28
Na zabibu, na mimea ya majani,
Barwani 80:28
29
Na mizaituni, na mitende,
Barwani 80:29
30
Na bustani zenye miti iliyo songana baraabara,
Barwani 80:30