1
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
2
Na kwa wanao toa kwa upole,
6
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
8
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
10
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
11
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
12
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
13
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
14
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
15
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
16
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
17
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
18
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
19
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
20
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
21
Lakini aliikadhibisha na akaasi.
22
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
23
Akakusanya watu akanadi.
24
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
25
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
26
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
27
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
28
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
29
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.
30
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
Sonraki 16 ayet →