Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Naziat 1 / 46
1
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
Barwani 79:1
2
Na kwa wanao toa kwa upole,
Barwani 79:2
3
Na wanao ogelea,
Barwani 79:3
4
Wakishindana mbio,
Barwani 79:4
5
Wakidabiri mambo.
Barwani 79:5
6
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
Barwani 79:6
7
Kifuate cha kufuatia.
Barwani 79:7
8
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
Barwani 79:8
9
Macho yatainama chini.
Barwani 79:9
10
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
Barwani 79:10
11
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
Barwani 79:11
12
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
Barwani 79:12
13
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
Barwani 79:13
14
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
Barwani 79:14
15
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
Barwani 79:15
16
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
Barwani 79:16
17
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
Barwani 79:17
18
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
Barwani 79:18
19
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
Barwani 79:19
20
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
Barwani 79:20
21
Lakini aliikadhibisha na akaasi.
Barwani 79:21
22
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
Barwani 79:22
23
Akakusanya watu akanadi.
Barwani 79:23
24
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
Barwani 79:24
25
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
Barwani 79:25
26
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
Barwani 79:26
27
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
Barwani 79:27
28
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
Barwani 79:28
29
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.
Barwani 79:29
30
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
Barwani 79:30