Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Nebe 1 / 40
1
WANAULIZANA nini?
Barwani 78:1
2
Ile khabari kuu,
Barwani 78:2
3
Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
Barwani 78:3
4
La! Karibu watakuja jua.
Barwani 78:4
5
Tena la! Karibu watakuja jua.
Barwani 78:5
6
Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
Barwani 78:6
7
Na milima kama vigingi?
Barwani 78:7
8
Na tukakuumbeni kwa jozi?
Barwani 78:8
9
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
Barwani 78:9
10
Na tukaufanya usiku ni nguo?
Barwani 78:10
11
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
Barwani 78:11
12
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
Barwani 78:12
13
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
Barwani 78:13
14
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
Barwani 78:14
15
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,
Barwani 78:15
16
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
Barwani 78:16
17
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
Barwani 78:17
18
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
Barwani 78:18
19
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,
Barwani 78:19
20
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
Barwani 78:20
21
Hakika Jahannamu inangojea!
Barwani 78:21
22
Kwa walio asi ndio makaazi yao,
Barwani 78:22
23
Wakae humo karne baada ya karne,
Barwani 78:23
24
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,
Barwani 78:24
25
Ila maji yamoto sana na usaha,
Barwani 78:25
26
Ndio jaza muwafaka.
Barwani 78:26
27
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
Barwani 78:27
28
Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
Barwani 78:28
29
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
Barwani 78:29
30
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
Barwani 78:30