Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Mürselat 1 / 50
1
Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!
Barwani 77:1
2
Na zinazo vuma kwa kasi!
Barwani 77:2
3
Na zikaeneza maeneo yote!
Barwani 77:3
4
Na zinazo farikisha zikatawanya!
Barwani 77:4
5
Na zinazo peleka mawaidha!
Barwani 77:5
6
Kwa kuudhuru au kuonya,
Barwani 77:6
7
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!
Barwani 77:7
8
Wakati nyota zitakapo futwa,
Barwani 77:8
9
Na mbingu zitakapo pasuliwa,
Barwani 77:9
10
Na milima itakapo peperushwa,
Barwani 77:10
11
Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,
Barwani 77:11
12
Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?
Barwani 77:12
13
Kwa siku ya kupambanua!
Barwani 77:13
14
Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?
Barwani 77:14
15
Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!
Barwani 77:15
16
Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?
Barwani 77:16
17
Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?
Barwani 77:17
18
Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!
Barwani 77:18
19
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
Barwani 77:19
20
Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?
Barwani 77:20
21
Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?
Barwani 77:21
22
Mpaka muda maalumu?
Barwani 77:22
23
Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.
Barwani 77:23
24
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
Barwani 77:24
25
Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya
Barwani 77:25
26
Walio hai na maiti?
Barwani 77:26
27
Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?
Barwani 77:27
28
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
Barwani 77:28
29
Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!
Barwani 77:29
30
Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!
Barwani 77:30