1
Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!
2
Na zinazo vuma kwa kasi!
3
Na zikaeneza maeneo yote!
4
Na zinazo farikisha zikatawanya!
5
Na zinazo peleka mawaidha!
6
Kwa kuudhuru au kuonya,
7
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!
8
Wakati nyota zitakapo futwa,
9
Na mbingu zitakapo pasuliwa,
10
Na milima itakapo peperushwa,
11
Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,
12
Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?
13
Kwa siku ya kupambanua!
14
Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?
15
Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!
16
Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?
17
Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?
18
Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!
19
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
20
Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?
21
Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?
23
Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.
24
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
25
Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya
27
Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?
28
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
29
Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!
30
Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!
Sonraki 20 ayet →