Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
İnsan 1 / 31
1
Hakika kilimpitia binaadamu kipindi katika zama ambacho kwamba hakuwa kitu kinacho tajwa.
Barwani 76:1
2
Hakika Sisi tumemuumba mtu kutokana na mbegu ya uhai iliyo changanyika, tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tukamfanya mwenye kusikia, mwenye kuona.
Barwani 76:2
3
Hakika Sisi tumembainishia Njia. Ama ni mwenye kushukuru, au mwenye kukufuru.
Barwani 76:3
4
Hakika Sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na Moto mkali.
Barwani 76:4
5
Hakika watu wema watakunywa katika vinywaji vilivyo changanyika na kafuri,
Barwani 76:5
6
Ni chemchem watakao inywa waja wa Mwenyezi Mungu, wakiifanya imiminike kwa wingi.
Barwani 76:6
7
Wanatimiza ahadi, na wanaiogopa siku ambayo shari yake inaenea sana,
Barwani 76:7
8
Na huwalisha chakula, juu ya kukipenda kwake, masikini, na yatima, na wafungwa.
Barwani 76:8
9
Hakika sisi tunakulisheni kwa wajihi wa Mwenyezi Mungu. Hatutaki kwenu malipo wala shukrani.
Barwani 76:9
10
Hakika sisi tunaiogopa kwa Mola wetu Mlezi hiyo siku yenye shida na taabu.
Barwani 76:10
11
Basi Mwenyezi Mungu atawalinda na shari ya siku hiyo, na atawakutanisha na raha na furaha.
Barwani 76:11
12
Na atawajazi Bustani za Peponi na maguo ya hariri kwa vile walivyo subiri.
Barwani 76:12
13
Humo wataegemea juu ya viti vya enzi, hawataona humo jua kali wala baridi kali.
Barwani 76:13
14
Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yataning'inia mpaka chini.
Barwani 76:14
15
Na watapitishiwa vyombo vya fedha na vikombe vya vigae,
Barwani 76:15
16
Vya fedha safi kama kiyoo, wamevipima kwa vipimo.
Barwani 76:16
17
Na humo watanyweshwa kinywaji kilicho changanyika na tangawizi.
Barwani 76:17
18
Hiyo ni chemchem iliyo humo inaitwa Salsabil.
Barwani 76:18
19
Na watawazungukia kuwatumikia wavulana wasio pevuka, ukiwaona utawafikiri ni lulu zilizo tawanywa.
Barwani 76:19
20
Na utakapo yaona, utakuwa umeona neema na ufalme mkubwa.
Barwani 76:20
21
Juu yao zipo nguo za hariri laini za kijani kibichi, na hariri nzito ya at'ilasi. Na watavikwa vikuku vya fedha, na Mola wao Mlezi atawanywesha kinywaji safi kabisa.
Barwani 76:21
22
Hakika haya ni malipo yenu; na juhudi zenu zimekubaliwa.
Barwani 76:22
23
Hakika Sisi tumekuteremshia Qur'ani kidogo kidogo.
Barwani 76:23
24
Basi ngojea hukumu ya Mola wako Mlezi wala usimt'ii miongoni mwao mwenye dhambi au mwenye kufuru.
Barwani 76:24
25
Na likumbuke jina la Mola wako Mlezi asubuhi na jioni;
Barwani 76:25
26
Na usiku msujudie Yeye, na umtakase usiku, wakati mrefu.
Barwani 76:26
27
Kwa hakika watu hawa wanapenda maisha ya kidunia, na wanaiacha nyuma yao siku nzito.
Barwani 76:27
28
Sisi tumewaumba, na tukavitia nguvu viungo vyao. Na tukitaka tutawabadilisha mfano wao wawe badala yao.
Barwani 76:28
29
Hakika haya ni mawaidha; basi anaye taka atashika Njia ya kwenda kwa Mola wake Mlezi.
Barwani 76:29
30
Wala hamwezi kutaka ila atakapo Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye ilimu, Mwenye hikima.
Barwani 76:30