Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Kıyame 1 / 40
1
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
Barwani 75:1
2
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
Barwani 75:2
3
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
Barwani 75:3
4
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
Barwani 75:4
5
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
Barwani 75:5
6
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
Barwani 75:6
7
Basi jicho litapo dawaa,
Barwani 75:7
8
Na mwezi utapo patwa,
Barwani 75:8
9
Na likakusanywa jua na mwezi,
Barwani 75:9
10
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
Barwani 75:10
11
La! Hapana pa kukimbilia!
Barwani 75:11
12
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
Barwani 75:12
13
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
Barwani 75:13
14
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
Barwani 75:14
15
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
Barwani 75:15
16
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
Barwani 75:16
17
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
Barwani 75:17
18
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
Barwani 75:18
19
Kisha ni juu yetu kuubainisha.
Barwani 75:19
20
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
Barwani 75:20
21
Na mnaacha maisha ya Akhera.
Barwani 75:21
22
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
Barwani 75:22
23
Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
Barwani 75:23
24
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
Barwani 75:24
25
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
Barwani 75:25
26
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
Barwani 75:26
27
Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
Barwani 75:27
28
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
Barwani 75:28
29
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
Barwani 75:29
30
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
Barwani 75:30