Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Müddessir 1 / 56
1
Ewe uliye jigubika!
Barwani 74:1
2
Simama uonye!
Barwani 74:2
3
Na Mola wako Mlezi mtukuze!
Barwani 74:3
4
Na nguo zako, zisafishe.
Barwani 74:4
5
Na yaliyo machafu yahame!
Barwani 74:5
6
Wala usitoe kwa kutaraji kuzidishiwa.
Barwani 74:6
7
Na kwa ajili ya Mola wako Mlezi, subiri!
Barwani 74:7
8
Basi litapo pulizwa barugumu,
Barwani 74:8
9
Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.
Barwani 74:9
10
Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.
Barwani 74:10
11
Niache peke yangu na niliye muumba;
Barwani 74:11
12
Na nikamjaalia awe na mali mengi,
Barwani 74:12
13
Na wana wanao onekana,
Barwani 74:13
14
Na nikamtgenezea mambo vizuri kabisa.
Barwani 74:14
15
Kisha anatumai nimzidishie!
Barwani 74:15
16
Hasha! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!
Barwani 74:16
17
Nitamtesa kwa mateso yasio wezekana.
Barwani 74:17
18
Kwani hakika yeye alifikiri na akapima.
Barwani 74:18
19
Basi ameangamia! Vipi alivyo pima!
Barwani 74:19
20
Tena ameangamia! Vipi alivyo pima!
Barwani 74:20
21
Kisha akatazama,
Barwani 74:21
22
Kisha akakunja kipaji, na akanuna.
Barwani 74:22
23
Kisha akaipa kisogo haki, na akatakabari.
Barwani 74:23
24
Na akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio nukuliwa.
Barwani 74:24
25
Haya si chochote ila kauli ya binaadamu.
Barwani 74:25
26
Nitakuja mtia kwenye Moto wa Saqar.
Barwani 74:26
27
Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto wa Saqar?
Barwani 74:27
28
Haubakishi wala hausazi.
Barwani 74:28
29
Unababua ngozi iwe nyeusi.
Barwani 74:29
30
Juu yake wapo kumi na tisa.
Barwani 74:30