Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Müzzemmil 1 / 20
1
Ewe uliye jifunika!
Barwani 73:1
2
Kesha usiku kucha, ila kidogo tu!
Barwani 73:2
3
Nusu yake, au ipunguze kidogo.
Barwani 73:3
4
Au izidishe - na soma Qur'ani kwa utaratibu na utungo.
Barwani 73:4
5
Hakika Sisi tutakuteremshia kauli nzito.
Barwani 73:5
6
Hakika kuamka usiku kunawafikiana zaidi na moyo, na maneno yake yanatua zaidi.
Barwani 73:6
7
Kwani hakika mchana una shughuli nyingi.
Barwani 73:7
8
Na lidhukuru jina la Mola wako Mlezi, na ujitolee kwake kwa ukamilifu.
Barwani 73:8
9
Mola Mlezi wa mashariki na magharibi, hapana mungu isipo kuwa Yeye, basi mfanye kuwa Mtegemewa wako.
Barwani 73:9
10
Na vumilia hayo wayasemayo, na jitenge nao kwa vizuri.
Barwani 73:10
11
Na niache Mimi na hao wanao kanusha, walio neemeka; na wape muhula kidogo!
Barwani 73:11
12
Hakika Sisi tunazo pingu nzito na Moto unao waka kwa ukali kabisa!
Barwani 73:12
13
Na chakula kinacho kwama kooni, na adhabu inayo umiza.
Barwani 73:13
14
Siku ambayo ardhi itatikiswa na milima pia, na milima itakuwa kama tifutifu la mchanga!
Barwani 73:14
15
Hakika Sisi tumemtuma kwenu Mtume aliye shahidi juu yenu, kama tulivyo mtuma Mtume kwa Firauni.
Barwani 73:15
16
Lakini Firauni alimuasi huyo Mtume, basi tukamshika mshiko wa mateso.
Barwani 73:16
17
Basi nyinyi mkikufuru, mtawezaje kujikinga na Siku ambayo itawafanya watoto wadogo waote mvi?
Barwani 73:17
18
Hapo mbingu zitapasuka! Ahadi yake itakuwa imetekelezwa.
Barwani 73:18
19
Kwa hakika hili ni kumbusho. Mwenye kutaka atashika njia ya kwendea kwa Mola wake Mlezi.
Barwani 73:19
20
Hakika Mola wako Mlezi anajua ya kuwa hakika wewe unakesha karibu na thuluthi mbili za usiku, na nusu yake, na thuluthi yake. Na baadhi ya watu walio pamoja nawe kadhaalika. Na Mwenyezi Mungu ndiye anaye ukadiria usiku na mchana. Anajua kuwa hamwezi kuweka hisabu, basi amekusameheni. Basi someni kilicho chepesi katika Qur'ani. Anajua ya kuwa baadhi yenu watakuwa wagonjwa, na wengine wanasafiri katika ardhi wakitafuta fadhila ya Mwenyezi Mungu, na wengine wanapigana katika Njia ya Mwenyezi Mungu. Kwa hivyo someni kilicho chepesi humo, na mshike Sala, na toeni Zaka, na mkopesheni Mwenyezi Mungu mkopo mwema. Na kheri yoyote mnayo itanguliza kwa ajili ya nafsi zenu mtaikuta kwa Mwenyezi Mungu, imekuwa bora zaidi, na ina thawabu kubwa sana. Na mtakeni msamaha Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
Barwani 73:20
Müzzemmil suresi tamamlandı