Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Nuh 1 / 28
1
Hakika Sisi tulimtuma Nuh'u kwa watu wake: Uwaonye kaumu yako kabla ya kuwafikia adhabu chungu.
Barwani 71:1
2
Akasema: Enyi watu wangu! Kwa hakika mimi ni mwonyaji wa dhaahiri kwenu,
Barwani 71:2
3
Ya kwamba mumuabudu Mwenyezi Mungu, na mumche Yeye, na mumt'ii.
Barwani 71:3
4
Atakughufirieni madhambi yenu, na atakuakhirisheni mpaka muda ulio wekwa. Hakika muda wa Mwenyezi Mungu utapo fika haucheleweshwi. Laiti mngejua!
Barwani 71:4
5
Akasema: Ee Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimewaita watu wangu usiku na mchana,
Barwani 71:5
6
Lakini wito wangu haukuwazidisha ila kukimbia.
Barwani 71:6
7
Na hakika mimi kila nilipo waita ili upate kuwaghufiria, walijiziba masikio yao kwa vidole vyao, na wakajigubika nguo zao, na wakakamia, na wakatakabari vikubwa mno!
Barwani 71:7
8
Tena niliwaita kwa uwazi,
Barwani 71:8
9
Kisha nikawatangazia kwa kelele, tena nikasema nao kwa siri.
Barwani 71:9
10
Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa kusamehe.
Barwani 71:10
11
Atakuleteeni mvua inyeshe mfululizo.
Barwani 71:11
12
Na atakupeni mali na wana, na atakupeni mabustani na atakufanyieni mito.
Barwani 71:12
13
Mna nini hamweki heshima ya Mwenyezi Mungu?
Barwani 71:13
14
Na hali Yeye kakuumbeni daraja baada ya daraja?
Barwani 71:14
15
Kwani hamwoni jinsi Mwenyezi Mungu alivyo ziumba mbingu saba kwa matabaka?
Barwani 71:15
16
Na akaufanya mwezi ndani yake uwe nuru, na akalifanya jua kuwa taa?
Barwani 71:16
17
Na Mwenyezi Mungu amekuotesheni katika ardhi kama mimea.
Barwani 71:17
18
Kisha atakurudsheni humo na atakutoeni tena.
Barwani 71:18
19
Na Mwenyezi Mungu amekukunjulieni ardhi kama busati.
Barwani 71:19
20
Ili mtembee humo katika njia zilizo pana.
Barwani 71:20
21
Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika hao wameniasi, na wamemfuata yule ambaye mali yake na wanawe hawakumzidishia ila khasara.
Barwani 71:21
22
Na wakapanga vitimbi vikubwa.
Barwani 71:22
23
Na wakasema: Msiwaache miungu yenu, wala msimwache Wadda wala Suwaa' wala Yaghutha, wala Yau'qa, wala Nasra.
Barwani 71:23
24
Na hao walikwisha wapoteza wengi, wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.
Barwani 71:24
25
Basi kwa ajili ya makosa yao waligharikishwa wakaingizwa Motoni, wala hawakuwapata wa kuwanusuru badala ya Mwenyezi Mungu.
Barwani 71:25
26
Na Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Usimwache juu ya ardhi mkaazi wake yeyote katika makafiri!
Barwani 71:26
27
Hakika ukiwaacha watawapoteza waja wako, wala wao hawatazaa ila waovu makafiri.
Barwani 71:27
28
Mola wangu Mlezi! Nighufirie mimi na wazazi wangu, na kila aliye ingia nyumbani mwangu kuwa ni mwenye kuamini, na Waumini wote wanaume, na Waumini wanawake. Na wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.
Barwani 71:28
Nuh suresi tamamlandı