Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Mearic 1 / 44
1
Muulizaji aliuliza juu ya adhabu itakayo tokea,
Barwani 70:1
2
Kwa makafiri - ambayo hapana awezaye kuizuia -
Barwani 70:2
3
Kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mwenye mbingu za daraja.
Barwani 70:3
4
Malaika na Roho hupanda kwendea kwake katika siku ambayo kadiri yake ni miaka khamsini elfu!
Barwani 70:4
5
Basi subiri kwa subira njema.
Barwani 70:5
6
Hakika wao wanaiona iko mbali,
Barwani 70:6
7
Na Sisi tunaiona iko karibu.
Barwani 70:7
8
Siku ambayo mbingu zitakapo kuwa kama maadeni iliyo yayushwa.
Barwani 70:8
9
Na milima itakuwa kama sufi.
Barwani 70:9
10
Wala jamaa hatamuuliza jamaa yake.
Barwani 70:10
11
Ijapo kuwa wataonyeshwa waonane. Atatamani mkosefu lau ajikomboe na adhabu ya siku hiyo kwa kuwatoa fidia wanawe,
Barwani 70:11
12
Na mkewe, na nduguye,
Barwani 70:12
13
Na jamaa zake walio kuwa wakimkimu,
Barwani 70:13
14
Na wote waliomo duniani, kisha aokoke yeye.
Barwani 70:14
15
La, hasha! Kwa hakika huo ni Moto mkali kabisa,
Barwani 70:15
16
Unao babua ngozi ya kichwa!
Barwani 70:16
17
Utamwita kila aliye geuza mgongo na akageuka.
Barwani 70:17
18
Na akakusanya mali, kisha akayahifadhi.
Barwani 70:18
19
Hakika mtu ameumbwa na papara.
Barwani 70:19
20
Inapo mgusa shari hupapatika.
Barwani 70:20
21
Na inapo mgusa kheri huizuilia.
Barwani 70:21
22
Isipo kuwa wanao sali,
Barwani 70:22
23
Ambao wanadumisha Sala zao,
Barwani 70:23
24
Na ambao katika mali yao iko haki maalumu
Barwani 70:24
25
Kwa mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba;
Barwani 70:25
26
Na ambao wanaisadiki Siku ya Malipo,
Barwani 70:26
27
Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao Mlezi.
Barwani 70:27
28
Hakika adhabu ya Mola wao Mlezi si ya kuaminika nayo.
Barwani 70:28
29
Na ambao wanahifadhi tupu zao.
Barwani 70:29
30
Isipo kuwa kwa wake zao, au iliyo wamiliki mikono yao ya kuume, basi hao hawalaumiwi -
Barwani 70:30