Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Hakka 1 / 52
1
Tukio la haki.
Barwani 69:1
2
Nini hilo Tukio la haki?
Barwani 69:2
3
Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?
Barwani 69:3
4
Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha.
Barwani 69:4
5
Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.
Barwani 69:5
6
Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.
Barwani 69:6
7
Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.
Barwani 69:7
8
Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?
Barwani 69:8
9
Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia.
Barwani 69:9
10
Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu.
Barwani 69:10
11
Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina,
Barwani 69:11
12
Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi.
Barwani 69:12
13
Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu,
Barwani 69:13
14
Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja,
Barwani 69:14
15
Siku hiyo ndio Tukio litatukia.
Barwani 69:15
16
Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.
Barwani 69:16
17
Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.
Barwani 69:17
18
Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.
Barwani 69:18
19
Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!
Barwani 69:19
20
Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.
Barwani 69:20
21
Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza,
Barwani 69:21
22
Katika Bustani ya juu,
Barwani 69:22
23
Matunda yake yakaribu.
Barwani 69:23
24
Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita.
Barwani 69:24
25
Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu!
Barwani 69:25
26
Wala nisingeli jua nini hisabu yangu.
Barwani 69:26
27
Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa.
Barwani 69:27
28
Mali yangu hayakunifaa kitu.
Barwani 69:28
29
Madaraka yangu yamenipotea.
Barwani 69:29
30
(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!
Barwani 69:30