Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Kalem 1 / 52
1
Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,
Barwani 68:1
2
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
Barwani 68:2
3
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.
Barwani 68:3
4
Na hakika wewe una tabia tukufu.
Barwani 68:4
5
Karibu utaona, na wao wataona,
Barwani 68:5
6
Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.
Barwani 68:6
7
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.
Barwani 68:7
8
Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.
Barwani 68:8
9
Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.
Barwani 68:9
10
Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,
Barwani 68:10
11
Mtapitapi, apitaye akifitini,
Barwani 68:11
12
Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,
Barwani 68:12
13
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
Barwani 68:13
14
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
Barwani 68:14
15
Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!
Barwani 68:15
16
Tutamtia kovu juu ya pua yake.
Barwani 68:16
17
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.
Barwani 68:17
18
Wala hawakusema: Mungu akipenda!
Barwani 68:18
19
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
Barwani 68:19
20
Likawa kama usiku wa giza.
Barwani 68:20
21
Asubuhi wakaitana.
Barwani 68:21
22
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
Barwani 68:22
23
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,
Barwani 68:23
24
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
Barwani 68:24
25
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
Barwani 68:25
26
Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!
Barwani 68:26
27
Bali tumenyimwa!
Barwani 68:27
28
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
Barwani 68:28
29
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
Barwani 68:29
30
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
Barwani 68:30