1
Litakapo tukia hilo Tukio
2
Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
3
Literemshalo linyanyualo,
4
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
5
Na milima itapo sagwasagwa,
6
Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
7
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
8
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
9
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
10
Na wa mbele watakuwa mbele.
11
Hao ndio watakao karibishwa
12
Katika Bustani zenye neema.
13
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
14
Na wachache katika wa mwisho.
15
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
16
Wakiviegemea wakielekeana.
17
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
18
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
19
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
20
Na matunda wayapendayo,
21
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.
23
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.
24
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
25
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,
26
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.
27
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?
28
Katika mikunazi isiyo na miba,
29
Na migomba iliyo pangiliwa,
30
Na kivuli kilicho tanda,
Sonraki 30 ayet →