Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Vakıa 1 / 96
1
Litakapo tukia hilo Tukio
Barwani 56:1
2
Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
Barwani 56:2
3
Literemshalo linyanyualo,
Barwani 56:3
4
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
Barwani 56:4
5
Na milima itapo sagwasagwa,
Barwani 56:5
6
Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
Barwani 56:6
7
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
Barwani 56:7
8
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
Barwani 56:8
9
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
Barwani 56:9
10
Na wa mbele watakuwa mbele.
Barwani 56:10
11
Hao ndio watakao karibishwa
Barwani 56:11
12
Katika Bustani zenye neema.
Barwani 56:12
13
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
Barwani 56:13
14
Na wachache katika wa mwisho.
Barwani 56:14
15
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
Barwani 56:15
16
Wakiviegemea wakielekeana.
Barwani 56:16
17
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
Barwani 56:17
18
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
Barwani 56:18
19
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
Barwani 56:19
20
Na matunda wayapendayo,
Barwani 56:20
21
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.
Barwani 56:21
22
Na Mahurulaini,
Barwani 56:22
23
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.
Barwani 56:23
24
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
Barwani 56:24
25
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,
Barwani 56:25
26
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.
Barwani 56:26
27
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?
Barwani 56:27
28
Katika mikunazi isiyo na miba,
Barwani 56:28
29
Na migomba iliyo pangiliwa,
Barwani 56:29
30
Na kivuli kilicho tanda,
Barwani 56:30