1
Arrah'man, Mwingi wa Rehema
5
Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
6
Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
7
Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
8
Ili msidhulumu katika mizani.
9
Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
10
Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
11
Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
12
Na nafaka zenye makapi, na rehani.
13
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
14
Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..
15
Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
16
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
17
Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
18
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
19
Anaziendesha bahari mbili zikutane;
20
Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.
21
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
22
Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.
23
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
24
Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.
25
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
26
Kila kilioko juu yake kitatoweka.
27
Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
28
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
29
Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.
30
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Sonraki 30 ayet →