Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Rahman 1 / 78
1
Arrah'man, Mwingi wa Rehema
Barwani 55:1
2
Amefundisha Qur'ani.
Barwani 55:2
3
Amemuumba mwanaadamu,
Barwani 55:3
4
Akamfundisha kubaini.
Barwani 55:4
5
Jua na mwezi huenda kwa hisabu.
Barwani 55:5
6
Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.
Barwani 55:6
7
Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,
Barwani 55:7
8
Ili msidhulumu katika mizani.
Barwani 55:8
9
Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.
Barwani 55:9
10
Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.
Barwani 55:10
11
Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.
Barwani 55:11
12
Na nafaka zenye makapi, na rehani.
Barwani 55:12
13
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Barwani 55:13
14
Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..
Barwani 55:14
15
Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.
Barwani 55:15
16
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha
Barwani 55:16
17
Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.
Barwani 55:17
18
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Barwani 55:18
19
Anaziendesha bahari mbili zikutane;
Barwani 55:19
20
Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.
Barwani 55:20
21
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Barwani 55:21
22
Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.
Barwani 55:22
23
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Barwani 55:23
24
Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.
Barwani 55:24
25
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Barwani 55:25
26
Kila kilioko juu yake kitatoweka.
Barwani 55:26
27
Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.
Barwani 55:27
28
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Barwani 55:28
29
Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.
Barwani 55:29
30
Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?
Barwani 55:30