Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Kamer 1 / 55
1
Saa imekaribia, na mwezi umepasuka!
Barwani 54:1
2
Na wakiona Ishara hugeuka upande na husema: Huu uchawi tu unazidi kuendelea.
Barwani 54:2
3
Na wamekanusha na wamefuata matamanio yao. Na kila jambo ni lenye kuthibiti.
Barwani 54:3
4
Na bila ya shaka zimewajia khabari zenye makaripio.
Barwani 54:4
5
Hikima kaamili; lakini maonyo hayafai kitu!
Barwani 54:5
6
Basi jiepushe nao. Siku atakapo ita mwitaji kuliendea jambo linalo chusha;
Barwani 54:6
7
Macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige walio tawanyika,
Barwani 54:7
8
Wanamkimbilia mwitaji, na makafiri wanasema: Hii ni siku ngumu.
Barwani 54:8
9
Kabla yao kaumu ya Nuhu walikanusha; wakamkanusha mja wetu, na wakasema ni mwendawazimu, na akakaripiwa.
Barwani 54:9
10
Basi akamwomba Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru!
Barwani 54:10
11
Basi tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayo miminika.
Barwani 54:11
12
Na tukazipasua ardhi kwa chemchem, yakakutana maji kwa jambo lilio kadiriwa.
Barwani 54:12
13
Na tukamchukua kwenye safina ya mbao na kamba.
Barwani 54:13
14
Ikawa inakwenda kwa nadhari yetu, kuwa ni malipo kwa alivyo kuwa amekanushwa.
Barwani 54:14
15
Na bila ya shaka tuliiacha iwe ni Ishara. Lakini je, yupo anaye kumbuka?
Barwani 54:15
16
Basi ilikuwaje adhabu yangu, na maonyo yangu.
Barwani 54:16
17
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani iwe nyepesi kufahamika. Lakini yupo anaye kumbuka?
Barwani 54:17
18
Kina A'di walikanusha. Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
Barwani 54:18
19
Hakika Sisi tuliwapelekea upepo wa kimbunga katika siku korofi mfululizo,
Barwani 54:19
20
Ukiwang'oa watu kama vigogo vya mitende vilio ng'olewa.
Barwani 54:20
21
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu?
Barwani 54:21
22
Na bila ya shaka Sisi tumeifanya Qur'ani nyepesi kufahamika; lakini yupo anaye kumbuka?
Barwani 54:22
23
Thamudi waliwakanusha Waonyaji.
Barwani 54:23
24
Wakasema: Ati tumfuate binaadamu mmoja katika sisi? Basi hivyo sisi tutakuwa katika upotofu na kichaa!
Barwani 54:24
25
Ni yeye tu aliye teremshiwa huo ukumbusho kati yetu sote? Bali huyu ni mwongo mwenye kiburi!
Barwani 54:25
26
Kesho watajua ni nani huyo mwongo mwenye kiburi.
Barwani 54:26
27
Hakika Sisi tutawapelekea ngamia jike ili kuwajaribu, basi watazame tu na ustahamili.
Barwani 54:27
28
Na waambie kwamba maji yatagawanywa baina yao; kila sehemu ya maji itahudhuriwa na aliye khusika.
Barwani 54:28
29
Basi wakamwita mtu wao akaja akamchinja.
Barwani 54:29
30
Basi ilikuwaje adhabu yangu na maonyo yangu!
Barwani 54:30