Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Necm 1 / 62
1
Naapa kwa nyota inapo tua,
Barwani 53:1
2
Mwenzenu huyu hakupotea, wala hakukosea.
Barwani 53:2
3
Wala hatamki kwa matamanio.
Barwani 53:3
4
Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa;
Barwani 53:4
5
Amemfundisha aliye mwingi wa nguvu,
Barwani 53:5
6
Mwenye kutua, akatulia,
Barwani 53:6
7
Naye yuko juu kabisa upeo wa macho.
Barwani 53:7
8
Kisha akakaribia na akateremka.
Barwani 53:8
9
Akawa ni kama baina ya mipinde miwili, au karibu zaidi.
Barwani 53:9
10
Akamfunulia mja wake (Mwenyezi Mungu) alicho mfunulia.
Barwani 53:10
11
Moyo haukusema uwongo uliyo yaona.
Barwani 53:11
12
Je! Mnabishana naye kwa aliyo yaona?
Barwani 53:12
13
Na akamwona mara nyingine,
Barwani 53:13
14
Penye Mkunazi wa mwisho.
Barwani 53:14
15
Karibu yake ndiyo ipo Bustani inayo kaliwa.
Barwani 53:15
16
Kilipo ufunika huo Mkunazi hicho kilicho ufunuika.
Barwani 53:16
17
Jicho halikuhangaika wala halikuruka mpaka.
Barwani 53:17
18
Kwa yakini aliona katika Ishara kubwa kabisa za Mola wake Mlezi.
Barwani 53:18
19
Je! Mmemuona Lata na Uzza?
Barwani 53:19
20
Na Manaat, mwingine wa tatu?
Barwani 53:20
21
Je! Nyinyi mnao wana wanaume na Yeye ndio awe na wanawake?
Barwani 53:21
22
Huo ni mgawanyo wa dhulma!
Barwani 53:22
23
Hayo hayakuwa ila ni majina mliyo wapa nyinyi na baba zenu. Mwenyezi Mungu hakuleta uthibitisho wowote juu ya hayo. Hawafuati ila dhana tu na kipendacho nafsi. Na kwa yakini uwongofu ulikwisha wafikia kutoka kwa Mola wao Mlezi.
Barwani 53:23
24
Ati mtu anakipata kila anacho kitamani?
Barwani 53:24
25
Mwenyezi Mungu tu ndiye Mwenye dunia na Akhera.
Barwani 53:25
26
Na wako Malaika wangapi mbinguni, ambao uombezi wao hautafaa chochote isipo kuwa baada ya Mwenyezi Mungu kutoa idhini kwa amtakaye na kumridhia.
Barwani 53:26
27
Hakika wasio amini Akhera bila ya shaka wao ndio wanawaita Malaika kwa majina ya kike.
Barwani 53:27
28
Nao hawana ujuzi wowote kwa hayo isipo kuwa wanafuata dhana tu. Na dhana haisaidii chochote mbele ya haki.
Barwani 53:28
29
Basi mwachilie mbali anaye upa kisogo ukumbusho wetu, na wala hataki ila maisha ya dunia.
Barwani 53:29
30
Huo ndio mwisho wao wa ujuzi. Hakika Mola wako Mlezi ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuipotea njia yake, na Yeye ndiye anaye mjua zaidi mwenye kuongoka.
Barwani 53:30