Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Tur 1 / 49
1
Naapa kwa mlima wa T'ur,
Barwani 52:1
2
Na Kitabu kilicho andikwa
Barwani 52:2
3
Katika ngozi iliyo kunjuliwa,
Barwani 52:3
4
Na kwa Nyumba iliyo jengwa,
Barwani 52:4
5
Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,
Barwani 52:5
6
Na kwa bahari iliyo jazwa,
Barwani 52:6
7
Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
Barwani 52:7
8
Hapana wa kuizuia.
Barwani 52:8
9
Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,
Barwani 52:9
10
Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
Barwani 52:10
11
Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,
Barwani 52:11
12
Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
Barwani 52:12
13
Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,
Barwani 52:13
14
(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!
Barwani 52:14
15
Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?
Barwani 52:15
16
Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.
Barwani 52:16
17
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,
Barwani 52:17
18
Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
Barwani 52:18
19
Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.
Barwani 52:19
20
Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.
Barwani 52:20
21
Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.
Barwani 52:21
22
Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.
Barwani 52:22
23
Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.
Barwani 52:23
24
Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.
Barwani 52:24
25
Wataelekeana wakiulizana.
Barwani 52:25
26
Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;
Barwani 52:26
27
Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.
Barwani 52:27
28
Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.
Barwani 52:28
29
Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.
Barwani 52:29
30
Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.
Barwani 52:30