1
Naapa kwa mlima wa T'ur,
2
Na Kitabu kilicho andikwa
3
Katika ngozi iliyo kunjuliwa,
4
Na kwa Nyumba iliyo jengwa,
5
Na kwa dari iliyo nyanyuliwa,
6
Na kwa bahari iliyo jazwa,
7
Hakika adhabu ya Mola wako Mlezi hapana shaka itatokea.
9
Siku zitakapo tikisika mbingu kwa mtikiso,
10
Na milima iwe inakwenda kwa mwendo mkubwa.
11
Basi ole wao siku hiyo hao wanao kadhibisha,
12
Ambao wanacheza katika mambo ya upuuzi.
13
Siku watapo sukumwa kwenye Moto kwa msukumo wa nguvu,
14
(Waambiwe): Huu ndio ule Moto mlio kuwa mkiukanusha!
15
Je! Huu ni uchawi, au hamwoni tu?
16
Uingieni, mkistahamili au msistahamili - ni mamoja kwenu. Hakika mnalipwa kwa mliyo kuwa mkiyatenda.
17
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na neema,
18
Wakifurahi kwa yale aliyo wapa Mola wao Mlezi. Na Mola wao Mlezi atawalinda na adhabu ya Motoni.
19
Kuleni na kunyweni kwa raha kabisa kwa sababu ya mliyo kuwa mkiyatenda.
20
Watakuwa wameegemea juu ya viti vya enzi vilivyo pangwa kwa safu. Na tutawaoza mahuru-l-aini.
21
Na walio amini na dhuriya zao wakawafuata kwa Imani tutawakutanisha nao dhuriya zao, na wala hatutawapunja hata kidogo katika vitendo vyao. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma.
22
Na tutawapa matunda, na nyama kama watavyo penda.
23
Watapeana humo bilauri zisio na vinywaji vya kuleta maneno ya upuuzi wala dhambi.
24
Iwe wanawapitia watumishi wao kama kwamba ni lulu zilizomo katika chaza.
25
Wataelekeana wakiulizana.
26
Waseme: Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa;
27
Basi Mwenyezi Mungu akatufanyia hisani na akatulinda na adhabu ya upepo wa Moto.
28
Hakika sisi zamani tulikuwa tukimwomba Yeye tu. Hakika Yeye ndiye Mwema Mwenye kurehemu.
29
Basi kumbusha! Kwani wewe, kwa neema ya Mola wako Mlezi, si kuhani wala mwendawazimu.
30
Au wanasema: Huyu ni mtunga mashairi, tunamtarajia kupatilizwa na dahari.
Sonraki 19 ayet →