Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Zariyat 1 / 60
1
Naapa kwa pepo zinazo tawanya,
Barwani 51:1
2
Na zinazo beba mizigo,
Barwani 51:2
3
Na zinazo kwenda kwa wepesi.
Barwani 51:3
4
Na zinazo gawanya kwa amri,
Barwani 51:4
5
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,
Barwani 51:5
6
Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.
Barwani 51:6
7
Naapa kwa mbingu zenye njia,
Barwani 51:7
8
Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.
Barwani 51:8
9
Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.
Barwani 51:9
10
Wazushi wameangamizwa.
Barwani 51:10
11
Ambao wameghafilika katika ujinga.
Barwani 51:11
12
Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?
Barwani 51:12
13
Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.
Barwani 51:13
14
Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.
Barwani 51:14
15
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
Barwani 51:15
16
Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.
Barwani 51:16
17
Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.
Barwani 51:17
18
Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.
Barwani 51:18
19
Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.
Barwani 51:19
20
Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.
Barwani 51:20
21
Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?
Barwani 51:21
22
Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.
Barwani 51:22
23
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.
Barwani 51:23
24
Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?
Barwani 51:24
25
Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.
Barwani 51:25
26
Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.
Barwani 51:26
27
Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?
Barwani 51:27
28
Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.
Barwani 51:28
29
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!
Barwani 51:29
30
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.
Barwani 51:30