Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Kaf 1 / 45
1
Qaaf. Naapa kwa Qur'ani tukufu!
Barwani 50:1
2
Bali wanastaajabu kwamba amewafikia mwonyaji kutoka miongoni mwao, na wakasema makafiri: Hili ni jambo la ajabu!
Barwani 50:2
3
Ati tukifa na tukawa udongo...? Kurejea huko kuko mbali!
Barwani 50:3
4
Hakika Sisi tunajua kiasi cha kila kinacho punguzwa na ardhi kutokana nao. Na kwetu kipo Kitabu kinacho hifadhi yote.
Barwani 50:4
5
Lakini waliikanusha Haki ilipo wajia; kwa hivyo wamo katika mambo ya mkorogo.
Barwani 50:5
6
Je! Hawaangalii mbingu zilizo juu yao! Vipi tulivyo zijenga, na tukazipamba. Wala hazina nyufa.
Barwani 50:6
7
Na ardhi tumeitandaza na tukaiwekea milima, na tukaiotesha mimea mizuri ya kila namna.
Barwani 50:7
8
Yawe haya ni kifumbua macho na ukumbusho kwa kila mja mwenye kuelekea.
Barwani 50:8
9
Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji yaliyo barikiwa, na kwa hayo tukaotesha mabustani na nafaka za kuvunwa.
Barwani 50:9
10
Na mitende mirefu yenye makole yaliyo zaa kwa wingi,
Barwani 50:10
11
Ili iwe ni riziki kwa waja wangu. Na tukaifufua kwa maji nchi iliyo kuwa imekufa. Kama hivyo ndivyo utakavyo kuwa ufufuaji.
Barwani 50:11
12
Kabla yao walikadhibisha kaumu ya Nuhu na wakaazi wa Rassi na Thamudi.
Barwani 50:12
13
Na A'di na Firauni na kaumu ya Lut'i.
Barwani 50:13
14
Na wakaazi wa Machakani, na watu wa Tubbaa'. Wote hao waliwakanusha Mitume, kwa hivyo onyo likathibitika juu yao.
Barwani 50:14
15
Kwani tulichoka kwa kuumba mara ya kwanza. Bali wao wamo katika shaka tu juu ya umbo jipya.
Barwani 50:15
16
Na hakika tumemuumba mtu, nasi tunayajua yanayo mpitikia katika nafsi yake. Na Sisi tuko karibu naye kuliko mshipa wa shingoni mwake.
Barwani 50:16
17
Wanapo pokea wapokeaji wawili, wanao kaa kuliani na kushotoni.
Barwani 50:17
18
Hatamki neno ila karibu yake yupo mwangalizi tayari.
Barwani 50:18
19
Na uchungu wa kutoka roho utamjia kwa haki. Hayo ndiyo uliyo kuwa ukiyakimbia.
Barwani 50:19
20
Na litapulizwa baragumu. Hiyo ndiyo Siku ya Miadi.
Barwani 50:20
21
Na kila nafsi itakuja na pamoja nayo mchungaji na shahidi.
Barwani 50:21
22
(Aambiwe): Kwa hakika ulikuwa umeghafilika na haya; basi leo tumekuondolea pazia lako, na kwa hivyo kuona kwako leo ni kukali.
Barwani 50:22
23
Na mwenzake atasema: Huyu niliye naye mimi kesha tayarishwa.
Barwani 50:23
24
Mtupeni katika Jahannamu kila kafiri mwenye inda,
Barwani 50:24
25
Akatazaye kheri, arukaye mipaka, mwenye kutia shaka,
Barwani 50:25
26
Aliye weka mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Basi mtupeni katika adhabu kali.
Barwani 50:26
27
Mwenzake aseme: Ee Mola wetu Mlezi! Sikumpoteza mimi, bali yeye mwenyewe alikuwa katika upotovu wa mbali.
Barwani 50:27
28
(Mwenyezi Mungu) aseme: Msigombane mbele yangu. Nilikuleteeni mbele onyo langu.
Barwani 50:28
29
Mbele yangu haibadilishwi kauli, wala Mimi siwadhulumu waja wangu.
Barwani 50:29
30
Siku tutapo iambia Jahannamu: Je! Umejaa? Nayo itasema: Je! Kuna ziada?
Barwani 50:30