Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Duhan 1 / 59
1
H'a Mim
Barwani 44:1
2
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,
Barwani 44:2
3
Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.
Barwani 44:3
4
Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,
Barwani 44:4
5
Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.
Barwani 44:5
6
Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
Barwani 44:6
7
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.
Barwani 44:7
8
Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.
Barwani 44:8
9
Lakini wao wanacheza katika shaka.
Barwani 44:9
10
Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,
Barwani 44:10
11
Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!
Barwani 44:11
12
Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.
Barwani 44:12
13
Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.
Barwani 44:13
14
Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.
Barwani 44:14
15
Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!
Barwani 44:15
16
Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.
Barwani 44:16
17
Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.
Barwani 44:17
18
Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.
Barwani 44:18
19
Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.
Barwani 44:19
20
Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.
Barwani 44:20
21
Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.
Barwani 44:21
22
Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.
Barwani 44:22
23
Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.
Barwani 44:23
24
Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa.
Barwani 44:24
25
Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!
Barwani 44:25
26
Na mimea na vyeo vitukufu!
Barwani 44:26
27
Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!
Barwani 44:27
28
Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.
Barwani 44:28
29
La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.
Barwani 44:29
30
Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,
Barwani 44:30