2
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,
3
Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.
4
Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,
5
Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.
6
Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
7
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.
8
Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.
9
Lakini wao wanacheza katika shaka.
10
Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,
11
Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!
12
Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.
13
Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.
14
Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.
15
Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!
16
Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.
17
Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.
18
Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.
19
Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.
20
Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.
21
Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.
22
Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.
23
Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.
24
Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa.
25
Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!
26
Na mimea na vyeo vitukufu!
27
Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!
28
Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.
29
La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.
30
Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,
Sonraki 29 ayet →