Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Zuhruf 1 / 89
1
H'a Mim
Barwani 43:1
2
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha.
Barwani 43:2
3
Hakika Sisi tumeifanya Qur'ani kwa Kiarabu ili mfahamu.
Barwani 43:3
4
Na hakika hiyo imo katika Asili ya Maandiko yalioko kwetu, ni tukufu na yenye hikima.
Barwani 43:4
5
Je! Tuache kukukumbusheni kabisa kwa kuwa nyinyi ni watu mlio pita mipaka kwa ukafiri?
Barwani 43:5
6
Na Manabii wangapi tuliwatuma kwa watu wa zamani!
Barwani 43:6
7
Na hawajii Nabii yeyote ila walikuwa wakimkejeli.
Barwani 43:7
8
Na tuliwaangamiza walio kuwa na nguvu kushinda wao. Na mfano wa watu wa zamani umekwisha pita.
Barwani 43:8
9
Na ukiwauliza: Nani aliye ziumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Kaziumba Mwenye nguvu, Mjuzi,
Barwani 43:9
10
Ambaye amekufanyieni ardhi kama tandiko, na akakufanyieni ndani yake njia mpate kuongoka.
Barwani 43:10
11
Na ambaye ndiye aliye teremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi, na kwa hayo tukaifufua nchi iliyo kufa. Na namna hivi ndivyo mtakavyo tolewa.
Barwani 43:11
12
Na ambaye ndiye aliye umba katika kila kitu jike na dume, na akakufanyieni marikebu na wanyama mnao wapanda.
Barwani 43:12
13
Ili mkae vizuri migongoni mwao, kisha mkumbuke neema za Mola wenu Mlezi mnapokaa sawa sawa juu yao na mseme: Ametakasika aliye mfanya huyu atutumikie, na tusingeli weza kufanya haya wenyewe.
Barwani 43:13
14
Na hakika sisi tutarudi kwa Mola wetu Mlezi.
Barwani 43:14
15
Na wanamfanyia katika waja wake fungu. Kwa hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila aliye dhaahiri.
Barwani 43:15
16
Au amejichukulia watoto wanawake katika vile alivyo viumba, na akakuteulieni nyinyi watoto wanaume?
Barwani 43:16
17
Na anapo bashiriwa mmoja wao kwa yale aliyo mpigia mfano Mwenyezi Mungu, uso wake husawijika na hujaa hasira.
Barwani 43:17
18
Ati aliye lelewa katika mapambo, na katika mabishano hawezi kusema kwa bayana...?
Barwani 43:18
19
Na wakawafanya Malaika, ambao ni waja wa Mwingi wa Rehema, ni wanawake! Kwani wameshuhudia kuumbwa kwao? Ushahidi wao utaandikwa na wao watahojiwa!
Barwani 43:19
20
Nao husema: Angeli penda Mwingi wa Rehema tusingeli waabudu sisi. Hawana ujuzi wowote wa hayo! Hawana ila kusema uwongo tu!
Barwani 43:20
21
Kwani tuliwapa Kitabu kabla ya hichi, na ikawa wao wanakishikilia hicho?
Barwani 43:21
22
Bali wanasema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, basi na sisi tunaongoza nyayo zao.
Barwani 43:22
23
Na kadhaalika hatukumtuma mwonyaji kwenye mji wowote ila watu wake walio deka kwa starehe walisema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, na sisi tunafuata nyayo zao.
Barwani 43:23
24
Akasema (Mwonyaji): Hata nikikuleteeni yenye uwongofu bora kuliko mlio wakuta nao baba zenu? Wakasema: Sisi tunayakataa tu hayo mliyo tumwa.
Barwani 43:24
25
Basi tukawalipizia. Angalia ulikuwaje mwisho wa walio kadhibisha!
Barwani 43:25
26
Na pale Ibrahim alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Hakika mimi ninajitenga mbali na hayo mnayo yaabudu,
Barwani 43:26
27
Isipo kuwa yule aliye niumba, kwani Yeye ataniongoa.
Barwani 43:27
28
Na akalifanya hili liwe neno lenye kubaki katika vizazi vyake ili warejee.
Barwani 43:28
29
Bali tuliwastarehesha hawa na baba zao mpaka ikawafikia Haki na Mtume aliye bainisha.
Barwani 43:29
30
Na ilipo wafikia Haki wakasema: Huu ni uchawi, na sisi hakika tunaukataa.
Barwani 43:30