Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Saffat 1 / 182
1
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
Barwani 37:1
2
Na kwa wenye kukataza mabaya.
Barwani 37:2
3
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
Barwani 37:3
4
Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
Barwani 37:4
5
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
Barwani 37:5
6
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
Barwani 37:6
7
Na kulinda na kila shet'ani a'si.
Barwani 37:7
8
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
Barwani 37:8
9
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
Barwani 37:9
10
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
Barwani 37:10
11
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
Barwani 37:11
12
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
Barwani 37:12
13
Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
Barwani 37:13
14
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
Barwani 37:14
15
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
Barwani 37:15
16
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
Barwani 37:16
17
Hata baba zetu wa zamani?
Barwani 37:17
18
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
Barwani 37:18
19
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
Barwani 37:19
20
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
Barwani 37:20
21
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
Barwani 37:21
22
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
Barwani 37:22
23
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
Barwani 37:23
24
Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:
Barwani 37:24
25
Mna nini? Mbona hamsaidiani?
Barwani 37:25
26
Bali hii leo, watasalimu amri.
Barwani 37:26
27
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
Barwani 37:27
28
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
Barwani 37:28
29
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
Barwani 37:29
30
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
Barwani 37:30