Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Yasin 1 / 83
1
Ya-Sin (Y. S.).
Barwani 36:1
2
Kwa Haki ya Qur'ani yenye hikima!
Barwani 36:2
3
Hakika wewe ni miongoni mwa walio tumwa,
Barwani 36:3
4
Juu ya Njia Iliyo Nyooka.
Barwani 36:4
5
Uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
Barwani 36:5
6
Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa, basi wao wamekuwa wenye kughafilika.
Barwani 36:6
7
Bila ya shaka kauli imekwisha thibiti juu ya wengi katika wao, kwa hivyo hawaamini.
Barwani 36:7
8
Tumeweka makongwa shingoni mwao, yakawafika videvuni. Kwa hivyo vichwa vyao viko juu tu.
Barwani 36:8
9
Tumeweka kizuizi mbele yao, na kizuizi nyuma yao, na tumewafunika macho yao; kwa hivyo hawaoni.
Barwani 36:9
10
Ni sawa sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini.
Barwani 36:10
11
Hakika wewe unamwonya mwenye kufuata ukumbusho, na akamcha Arrahman, Mwingi wa Rehema, kwa ghaibu. Basi mbashirie huyo msamaha na ujira mwema.
Barwani 36:11
12
Hakika Sisi tunawafufua wafu, na tunayaandika wanayo yatanguliza, na wanayo yaacha nyuma. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asli lenye kubainisha.
Barwani 36:12
13
Na wapigie mfano wa wakaazi wa mji walipo wafikia walio tumwa.
Barwani 36:13
14
Tulipo watumia wawili, wakawakanusha. Basi tukawazidishia nguvu kwa mwingine wa tatu. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwenu.
Barwani 36:14
15
Wakasema: Nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na Mwingi wa Rehema hakuteremsha kitu. Nyinyi mnasema uwongo tu.
Barwani 36:15
16
Wakasema: Mola wetu Mlezi anajua kwamba hakika sisi tumetumwa kwenu.
Barwani 36:16
17
Wala si juu yetu ila kufikisha ujumbe ulio wazi.
Barwani 36:17
18
Wakasema: Sisi tumeagua kuwa nyinyi ni wakorofi. Ikiwa hamtaacha basi kwa yakini tutakupigeni mawe, na mtapata adhabu chungu kutoka kwetu.
Barwani 36:18
19
Wakasema: Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu walio pindukia mipaka.
Barwani 36:19
20
Na akaja mtu mbio kutokea upande wa mbali wa mjini, akasema: Enyi watu wangu! Wafuateni hawa walio tumwa.
Barwani 36:20
21
Wafuateni ambao hawakutakini ujira, hali ya kuwa wenyewe wameongoka.
Barwani 36:21
22
NA KWA NINI nisimuabudu yule aliye niumba na kwake mtarejeshwa?
Barwani 36:22
23
Je! Niishike miungu mingine badala yake? Arrahmani, Mwingi wa Rehema, akinitakia madhara uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa.
Barwani 36:23
24
Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhaahiri.
Barwani 36:24
25
Hakika mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni!
Barwani 36:25
26
Akaambiwa: Ingia Peponi! Akasema: Laiti kuwa watu wangu wangeli jua
Barwani 36:26
27
Jinsi Mola wangu Mlezi alivyo nisamehe, na akanifanya miongoni mwa walio hishimiwa.
Barwani 36:27
28
Na hatukuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala si wenye kuteremsha.
Barwani 36:28
29
Hakukuwa ila ukelele mmoja tu; na mara walizimwa!
Barwani 36:29
30
Nawasikitikia waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli.
Barwani 36:30