Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Şuara 1 / 227
1
T'aa Siin Miim. (T'. S. M.)
Barwani 26:1
2
Hizi ni Aya za Kitabu kinacho bainisha.
Barwani 26:2
3
Huenda labda ukajikera nafsi yako kwa kuwa hawawi Waumini.
Barwani 26:3
4
Tunge penda tungeli wateremshia kutoka mbinguni Ishara zikanyenyekea shingo zao.
Barwani 26:4
5
Wala hauwafikii ukumbusho mpya kutoka kwa Arrahman ila wao hujitenga nao.
Barwani 26:5
6
Kwa yakini wamekanusha; kwa hivyo zitakuja wafikia khabari za yale waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.
Barwani 26:6
7
Je! Hawakuiona ardhi, mimea mingapi tumeiotesha humo, ya kila namna nzuri?
Barwani 26:7
8
Hakika katika haya zipo Ishara. Lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.
Barwani 26:8
9
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.
Barwani 26:9
10
Na Mola wako Mlezi, alipo mwita Musa, akamwambia: Fika kwa watu madhaalimu,
Barwani 26:10
11
Watu wa Firauni. Hawaogopi?
Barwani 26:11
12
Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe.
Barwani 26:12
13
Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun.
Barwani 26:13
14
Na wao wana kisasi juu yangu, kwa hivyo naogopa wasije kuniuwa.
Barwani 26:14
15
Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza.
Barwani 26:15
16
Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Barwani 26:16
17
Waachilie Wana wa Israili wende nasi.
Barwani 26:17
18
(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?
Barwani 26:18
19
Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?
Barwani 26:19
20
(Musa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea.
Barwani 26:20
21
Basi nikakukimbieni nilipo kuogopeni, tena Mola wangu Mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa Mitume.
Barwani 26:21
22
Na hiyo ndiyo neema ya kunisumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?
Barwani 26:22
23
Firauni akasema: Na nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?
Barwani 26:23
24
Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini.
Barwani 26:24
25
(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?
Barwani 26:25
26
(Musa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza.
Barwani 26:26
27
(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu.
Barwani 26:27
28
(Musa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na viliomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini.
Barwani 26:28
29
(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani.
Barwani 26:29
30
Akasema: Je! Ijapo kuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?
Barwani 26:30