Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Müminun 1 / 118
1
HAKIKA wamefanikiwa Waumini,
Barwani 23:1
2
Ambao ni wanyenyekevu katika Sala zao,
Barwani 23:2
3
Na ambao hujiepusha na mambo ya upuuzi,
Barwani 23:3
4
Na ambao wanatoa Zaka,
Barwani 23:4
5
Na ambao wanazilinda tupu zao,
Barwani 23:5
6
Isipo kuwa kwa wake zao au kwa iliyo wamiliki mikono yao ya kulia. Kwani hao si wenye kulaumiwa.
Barwani 23:6
7
Lakini anaye taka kinyume cha haya, basi hao ndio warukao mipaka.
Barwani 23:7
8
Na ambao wanazitimiza amana zao na ahadi zao,
Barwani 23:8
9
Na ambao Sala zao wanazihifadhi -
Barwani 23:9
10
Hao ndio warithi,
Barwani 23:10
11
Ambao watairithi Pepo ya Firdausi, wadumu humo.
Barwani 23:11
12
Na kwa yakini tumemuumba mtu kutokana na asli ya udongo.
Barwani 23:12
13
Kisha tukamjaalia awe tone ya mbegu ya uzazi katika kalio madhubuti.
Barwani 23:13
14
Kisha tukaiumba tone kuwa damu iliyo ganda, na tukaiumba damu kuwa pande la nyama, kisha tukaliumba pande la nyama kuwa mifupa, na mifupa tukaivika nyama. Kisha tukamfanya kiumbe mwengine. Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.
Barwani 23:14
15
Kisha hakika nyinyi baada ya hayo mtakufa.
Barwani 23:15
16
Kisha hakika nyinyi Siku ya Kiyama mtafufuliwa.
Barwani 23:16
17
Na kwa yakini tumeziumba juu yenu njia saba. Nasi hatukuwa wenye kughafilika na viumbe.
Barwani 23:17
18
Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi na tukayatuliza katika ardhi. Na hakika Sisi tunaweza kuyaondoa.
Barwani 23:18
19
Kwa maji hayo tukakufanyieni bustani za mitende na mizabibu, mnapata humo matunda mengi, na katika hayo mnakula;
Barwani 23:19
20
Na mti utokao katika mlima wa Sinai, unatoa mafuta na kuwa kitoweo kwa walao.
Barwani 23:20
21
Na hakika mnayo mazingatio makubwa katika nyama hoa - tunakunywesheni katika vile viliomo matumboni mwao, na nyinyi mnapata katika hao manufaa mengi, na pia mnawala.
Barwani 23:21
22
Na juu yao na juu ya marikebu mnabebwa.
Barwani 23:22
23
Na hakika tulimtuma Nuhu kwa watu wake, akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni Mwenyezi Mungu. Nyinyi hamna mungu asiye kuwa Yeye. Basi je! Hamwogopi?
Barwani 23:23
24
Walisema wale wakuu walio kufuru katika watu wake: Huyu si chochote ila ni mtu tu kama nyinyi. Anataka kujipa ubora juu yenu. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu amependa basi yakini angeli teremsha Malaika. Hatukusikia haya kwa baba zetu wa zamani.
Barwani 23:24
25
Huyu si lolote ila ni mtu mwenye wazimu. Basi mngojeeni tu kwa muda.
Barwani 23:25
26
Akasema (Nuhu): Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwa kuwa wamenikanusha.
Barwani 23:26
27
Tukampa wahyi: Unda jahazi mbele ya macho yetu na uwongozi wetu! Basi itapo fika amri yetu na ikafurika tanuri, hapo waingize ndani yake wa kila namna dume na jike, na ahali zako, isipo kuwa yule ambaye katika wao juu yake imekwisha tangulia kauli. Wala usinitajie hao walio dhulumu. Kwani hao bila ya shaka watazamishwa.
Barwani 23:27
28
Basi utakapo tulia wewe na walio pamoja nawe humo marikebuni, sema: Alhamdulillahi Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, aliye tuokoa na watu madhaalimu!
Barwani 23:28
29
Na sema: Mola wangu Mlezi! Niteremshe mteremsho wenye baraka, na Wewe ni Mbora wa wateremshaji.
Barwani 23:29
30
Hakika katika hayo yapo mazingatio. Na kwa yakini Sisi ni wenye kuwafanyia mtihani.
Barwani 23:30