Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Ta Ha 1 / 135
1
T'AHA!
Barwani 20:1
2
Hatukukuteremshia Qur'ani ili upate mashaka.
Barwani 20:2
3
Bali ni mawaidha kwa wenye kunyenyekea.
Barwani 20:3
4
Materemsho yatokayo kwa aliye umba ardhi na mbingu zilizo juu.
Barwani 20:4
5
Arrahmani, Mwingi wa Rehema, aliye tawala juu ya Kiti cha Enzi.
Barwani 20:5
6
Ni vyake vyote viliomo mbinguni na viliomo katika ardhi, na viliomo baina yao, na viliomo chini ya ardhi.
Barwani 20:6
7
Na ukinyanyua sauti kwa kusema... basi hakika Yeye anajua siri na duni kuliko siri.
Barwani 20:7
8
Mwenyezi Mungu! Hapana mungu isipo kuwa Yeye. Yeye ana majina mazuri kabisa.
Barwani 20:8
9
Na je! Imekufikia hadithi ya Musa?
Barwani 20:9
10
Alipo uona moto, akawaambia watu wake: Ngojeni! Mimi nimeuona moto, huenda nikakuleteeni kijinga kutoka huo moto, au nikapata uongofu kwenye moto.
Barwani 20:10
11
Basi alipo ufikia akaitwa: Ewe Musa!
Barwani 20:11
12
Hakika Mimi ndiye Mola wako Mlezi! Basi vua viatu vyako. Kwani upo katika bonde takatifu la T'uwa.
Barwani 20:12
13
Nami nimekuteua wewe; basi sikiliza unayo funuliwa.
Barwani 20:13
14
Hakika Mimi ndiye Mwenyezi Mungu. Hapana mungu ila Mimi tu. Basi niabudu Mimi, na ushike Sala kwa ajili ya kunikumbuka Mimi.
Barwani 20:14
15
Hakika Saa itakuja bila ya shaka. Nimekaribia kuificha, ili kila nafsi ilipwe kwa iliyo yafanya.
Barwani 20:15
16
Kwa hivyo asikukengeushe nayo yule ambaye haiamini na akafuata pumbao lake ukaja kuhiliki.
Barwani 20:16
17
Na nini hicho kilichomo mkononi mwako wa kulia, ewe Musa?
Barwani 20:17
18
Akasema: Hii ni fimbo yangu; naiegemea na ninawaangushia majani kondoo na mbuzi wangu. Tena inanifaa kwa matumizi mengine.
Barwani 20:18
19
Akasema: Itupe, ewe Musa!
Barwani 20:19
20
Akaitupa. Mara ikawa nyoka anaye kwenda mbio.
Barwani 20:20
21
Akasema: Ikamate, wala usiogope! Tutairudisha hali yake ya kwanza.
Barwani 20:21
22
Na uambatishe mkono wako kwenye ubavu. Utatoka mweupe pasipo kuwa na madhara yoyote. Hiyo ni ishara nyengine.
Barwani 20:22
23
Ili tukuonyeshe baadhi ya ishara zetu kubwa.
Barwani 20:23
24
Nenda kwa Firauni; kwani hakika yeye amepindukia mipaka.
Barwani 20:24
25
(Musa) akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Nikunjulie kifua changu,
Barwani 20:25
26
Na unifanyie nyepesi kazi yangu,
Barwani 20:26
27
Na ulifungue fundo lililo katika ulimi wangu,
Barwani 20:27
28
Wapate kufahamu maneno yangu.
Barwani 20:28
29
Na nipe waziri katika watu wangu,
Barwani 20:29
30
Harun, ndugu yangu.
Barwani 20:30