1
Alif Lam Ra. (A. L. R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur'ani inayo bainisha.
2
HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.
3
Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.
4
Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.
5
Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.
6
Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.
7
Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?
8
Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.
9
Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.
10
Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo.
11
Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli.
12
Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu.
13
Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale.
14
Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda,
15
Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa.
16
Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.
17
Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye.
18
Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana.
19
Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi chake.
20
Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.
21
Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa kipimo maalumu.
22
Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.
23
Na Sisi ndio tunao huisha na tunao fisha. Na Sisi ndio Warithi.
24
Na tunawajua walio tangulia katika nyinyi, na tunawajua walio taakhari.
25
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mjuzi.
26
Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
27
Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.
28
Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
29
Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia.
30
Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,
Sonraki 30 ayet →