Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Hicr 1 / 99
1
Alif Lam Ra. (A. L. R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur'ani inayo bainisha.
Barwani 15:1
2
HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.
Barwani 15:2
3
Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.
Barwani 15:3
4
Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.
Barwani 15:4
5
Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.
Barwani 15:5
6
Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.
Barwani 15:6
7
Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?
Barwani 15:7
8
Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.
Barwani 15:8
9
Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.
Barwani 15:9
10
Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo.
Barwani 15:10
11
Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli.
Barwani 15:11
12
Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu.
Barwani 15:12
13
Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale.
Barwani 15:13
14
Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda,
Barwani 15:14
15
Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa.
Barwani 15:15
16
Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.
Barwani 15:16
17
Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye.
Barwani 15:17
18
Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana.
Barwani 15:18
19
Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi chake.
Barwani 15:19
20
Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.
Barwani 15:20
21
Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa kipimo maalumu.
Barwani 15:21
22
Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.
Barwani 15:22
23
Na Sisi ndio tunao huisha na tunao fisha. Na Sisi ndio Warithi.
Barwani 15:23
24
Na tunawajua walio tangulia katika nyinyi, na tunawajua walio taakhari.
Barwani 15:24
25
Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mjuzi.
Barwani 15:25
26
Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
Barwani 15:26
27
Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.
Barwani 15:27
28
Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.
Barwani 15:28
29
Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia.
Barwani 15:29
30
Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,
Barwani 15:30