Ana SayfaMealler › Barwani
B

Barwani

Barwani
Barwani meali ile okumaya başla
Adiyat 1 / 11
1
Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,
Barwani 100:1
2
Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,
Barwani 100:2
3
Wakishambulia wakati wa asubuhi,
Barwani 100:3
4
Huku wakitimua vumbi,
Barwani 100:4
5
Na wakijitoma kati ya kundi,
Barwani 100:5
6
Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!
Barwani 100:6
7
Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
Barwani 100:7
8
Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
Barwani 100:8
9
Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
Barwani 100:9
10
Na yakakusanywa yaliomo vifuani?
Barwani 100:10
11
Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!
Barwani 100:11
Adiyat suresi tamamlandı